Hongera Kingwendu Umepigana!



RASHID Mwinshehe Mzange ‘Kingwendu’ mgombea wa Ubunge kupitia CUF aliyekuwa akiungwa mkono na UKAWA afanya kazi nzuri baada ya kupata kura takribani 8,000 nyuma ya Mbunge aliyekuwa akitetea jimbo hilo kupitia chama cha CCM ndugu Seleiman Jafo.



Kingwendu ambaye ni msanii wa vichekesho Swahilihood ambaye ni kivutio katika tasnia ya filamu aliweza kuingia katika medani za kisiasa kuwania jimbo la Kisarawe kwa kujiamini kabisa bila uoga anastahili pongezi kama msanii.

Amaeleta upinzani kwa mwanasiasa mkongwe wengi wangetegemea kukosa kabisa kura lakini kuna watu wamemwelewa, kwa maana nyingine siku zijazo anaweza kuleta upinzani na kuwainua wasanii wengine.

Msanii huyo anajipanga zaidi ili wakati ukifika ataingia tena katika kinyang’anyiro cha cheo chochote cha kisiasa tayari ameanza na spidi hiyo ataendeleza katika kutafuta nafasi ya kuwatumikia wakazi wa Kisarawe.

Filamu Central